RC KUNENGE AFANYA ZIARA HOSPITALI YA WILAYA MSOGA
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhe Abubakar Kunenge hii leo ameanya ziara maalumu katika hospital ya Msoga kwa lengo la kukagua na kuona maendeleo ya Jengo la dhararu la (EMD) Iliyopo katika hospital ya Msoga . Akiwa katika hospitali hiyo Mhe Kunenge alipata kuona maendelea ujenzi wa jengo la hilo la dharura ambalo ujenzi huo umekamilia kwa asimilia kubwa na kilichobaki ni umalizaji wa uwekezaji wa samani,Ujenzi wa majengo mbalimbali katika hospitali hiyo Pamoja na eneo linalotarajiwa kujengwa uwanja wa kisasa wa Mpira wa miguu. Katika ziara hiyo Mhe Kunenge alipata wasaa wa kusalimiana na kuzungumza na wananchi waliofika katika hospitali ya Msoga kupata huduma ambapo alisema alitembelea hospitali hiyo kuona maendeleo ya ujenzi lakini pia kuona namna huduma zinazotolewa hospitalini hapo. ''Nimekuja kuona Maendeleo ya ujenzi wa jengo ya huduma za dharura lakini pia kuona jinsi utoaji wa huduma unavyoendelea na naamini ninyi ndiyo mtawaambia huduma ina ubora ama sivyo”.Amesema Mhe.Kuneng...